Jumanne , 5th Sep , 2017

Mwenyekiti wa CHAUMMA, Hashim Rungwe Spunda anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo kikuu cha polisi cha Kanda maalum ya Dar es Salaam kwa takribani siku nne sasa

Kamanda Lazaro Mambosasa amethibitisha taarifa hizo bila ya kutaja sababu zilizopelekea Mhe, Rungwe kukamatwa kwake

Rungwe ambaye alikuwa miongoni mwa wagombea urais wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, pia amekuwa miongoni mwa wanasiasa ambao wamekuwa wakiikosoa serikali mara kwa mara katika utendaji kazi wake, na hivi karibuni aliitaka serikali imalize mgogoro na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd iliyozuia ndege aina ya bombardier Q400- Dash 8 iliyonunuliwa nchini Canada.