Alhamisi , 8th Mei , 2014

Jumuiya ya Ulaya imeisadia Jumuiya ya Afrika Mashariki kiasi cha EURO Milion 2.3 kwa ajili ya kuimarisha ulinzi katika ukanda  wa bahari ya Hindi.

 Balozi wa umoja wa Ulaya hapa nchini Tanzania Bw. Filiberto  Sebregondi

Mwenyekiti wa  mfuko  wa   sekta binafsi  nchini   Dkt. Regnald Mengi  amesema itakuwa vigumu kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kukuza uchumi kama hazitadhibiti tatizo sugu la Rushwa  linaloendelea kujikita katika sekta mbalimbali.
 
Dr. Mengi ameyasema hayo jijini Arusha katika hafla ya utiaji saini mkataba wa   msaada   wa   Euro Milioni 2.3 zilizotolewa na Jumuiya ya Ulaya kwa ajili ya kuimarisha ulinzi katika ukanda  wa bahari ya Hindi.
 
Dr. Mengi ambaye  pia ni Mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP amesema  tatizo la rushwa  limeendelea kushika kasi  na  udhibiti wake unaendelea kuwa mgumu kutokana na utaratibu unaotumika kulishughulikia  ambao umejikita zaidi kwa wanaotoa na kwa watu wadogo wadogo  .
 
Kwa upande wake mwenyekiti  wa baraza  la wafanyabiashara  Afrika  Mashariki Bw. Felexs  Mosha  na  mwenyekiti  wa watendaji   wakuu    wa   makampuni    nchini  Bw Ally  Mafuruku   Wamesema  pia  nchi za      wanachama   wa   jumuiya   hiyo   zinakabiliwa na tatizo  la  gharama  kubwa  za  uwekezaji  na  ukosefu  wa taarifa  muhimu.
 
Naye  naibu  katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia fedha na utawala Jean Cloude  amesema  msaada  huo  wa  Jumuiya ya   Ulaya   utasaidia  kuimarisha   ulinzi   hasa  eneo  la  bahari  ya  Hindi ,
 
 Balozi wa umoja wa Ulaya hapa nchini  Bw. Filiberto  Sebregondi  pamoja   na  kuelezea   azma   ya   Jumuiya   ya   Ulaya   ya   kuendelea   kuisadia   Jumuiya   ya   Afrika  Mashariki   amesema   pamoja  na  changamoto  zinazojitokeza    zikishughulikiwa  upo  uwezekano.
 
Msaada  huo   wa   Euro Milioni 2.3  kutoka Jumuiya  ya  Ulaya   (EU) ni   mwendelezo  wa   kampeni   za  Jumuiya  hiyo  kuisadia  Jumuiya  ya  Afrika  Mashariki   ambapo  kwa
kipindi cha mwaka 2010 kiasi cha Euro Milion 37.5  zimetolwa.