Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

CORONA: Hadithi ya mapambano isiyoisha utamu

Jumatano , 30th Dec , 2020

Machi 16, 2020, Tanzania ilithibitisha kisa cha kwanza cha mgonjwa wa Corona, taarifa ambayo ilitolewa na Waziri wa Afya wa wakati huo Ummy Mwalimu, ambaye alisema kuwa mgonjwa ni mwanamke raia wa Tanzania aliyewasili nchini Machi 15 kupitia uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanajaro.

Kushoto ni Rais Dkt. John Magufuli, na kulia ni kipimo cha COVID-19

Taarifa ya Waziri Ummy, ilieleza kuwa mgonjwa huyo aliwasili na ndege ya shirika la Rwanda akitokea nchini Ubelgiji, ikiwa ni moja ya Taifa ambalo lilikuwa limeathirika na virusi hivyo kwa kiasi kikubwa.

Mara baada ya mgonjwa wa kwanza kuthibitika nchini, Machi 17, 2020, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alitangaza kufunga shule kwa muda wa siku 30, pamoja na kuzuia mikusanyiko mbalimbali ikiwemo matamasha na michezo, mikutano mbalimbali ikiwemo ya shughuli za kisiasa, jambo ambalo lilikuwa ni kama tahadhari za kujikinga na kusambaa kwa maambukizi ya virusi hivyo.

Mbali na serikali kuchukua hatua hizo, Serikali pia ilijipanga kwa uhakika kwa kuweka mazingira ya kukabiliana na ugonjwa huo ikiwemo kutenga hospitali maalum za Mloganzila ya Dar es Salaam, kituo cha Buswelu (Mwanza) na Hospitali ya Mawenzi (Kilimanjaro), Mnazi Mmoja (Zanzibar) na ChakeChake (Pemba) kwa ajili ya kutoa huduma kwa waathirika wa ugonjwe huo.

Safari ya kuchukua tahadhari ikaanza rasmi kwa Watanzania, ikiwemo uvaaji wa barakoa, kuepuka mikusanyiko, unawaji wa mikono, utumiaji wa vitakasa mikono huku nguvu kubwa ikiwekezwa kwenye maombi.

Aprili 16, 2020, kupitia ukurasa wake wa mtandao wa twitter, Rais Dkt. Magufuli, aliwataka Watanzania kutenga muda wa siku tatu kwa ajili ya dua na sala zao kwa Mwenyezi Mungu ili aweze kuliponya Taifa na janga hilo ambalo hata sasa bado linasumbua Mataifa mengi Duniani.

Aprili 22, 2020, Rais Magufuli, aliwahutubia Watanzania akiwa Chato Geita, na kuwatoa hofu waliyonayo kuhusu ugonjwa huo, ambapo alizuia masuala ya 'lockdown' kama ambavyo watu wengi walipendekeza kwa kipindi hicho na kueleza kuwa siyo wote wanaofariki dunia ni kutokana na ugonjwa bali wengine wanafariki kutokana na hofu waliyonayo.

Kauli hiyo ya Rais Dkt. Magufuli, iliamsha matumaini ya Watanzania yaliyokuwa yamelala, ilirejesha tumaini jipya na mwangaza kwenye nyuso za watu wengi waliokuwa hawana matumaini, hii yote ni kulingana na takwimu za maambukizi na vifo vya watu kutoka katika maeneo mbalimbali Duniani.

Mbali na Dkt. Rais Magufuli, kuzuia 'lockdown' kama ambavyo mataifa mbalimbali Duniani yalikuwa yamekwishachukua hatua za kuwafungia wananchi wake ndani, yeye pia alisisitiza suala la matumizi ya tiba mbadala ikiwemo kujifukiza na kupiga nyungu.

Mpaka sasa Watanzania wengi na mataifa mengi Duniani, wamekuwa wakimpongeza Rais Magufuli, kwa kauli yake ya kishujaa kwani yeye aliamua kuwa mstari wa mbele katika mapambano hayo licha ya wananchi wake kuendelea kuchukua tahadhari za ugonjwa huo, lakini kauli yake moja tu ndiyo ilikuwa tiba na kupelekea mpaka sasa Tanzania haijatangaza tena kisa kipya cha mgonjwa wa COVID-19.

Ugonjwa wa Virusi vya Corona (COVID-19), ulianzia nchini China mwishoni mwa mwaka 2019, na kusambaa Mataifa mbalimbali Duniani.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita