Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Fahamu aliyoyaacha Mama Rwakatare

Jumatano , 30th Dec , 2020

Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Moto Assemblies of God,  Askofu Dkt. Gertrude Rwakatare, alifariki dunia Alfajiri ya Aprili 20, 2020, katika hospitali ya Rabininsia iliyopo jijini Dar es Salaam baada ya kuugua maradhi ya moyo.

Marehemu Askofu Dkt. Gertrude Rwakatare, wakati wa uhai wake.

Taarifa ya kifo cha Mama Rwakatare ilitolewa mapema na mwanaye wa kiume Mutta Rwakatare, alipozungumza kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio, taarifa ambayo baadaye pia ilitolewa na Spika wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai.

Mama Rwakatare alizaliwa Desemba 31, 1950, huko Ifakara mkoani Morogoro, na alisoma Shule ya Msingi Ifakara, akajiunga na Sekondari ya Korogwe hadi kidato cha sita na baadaye alijiunga na Chuo cha North London Polytechnic nchini Uingereza na baadaye pia alijiunga na Chuo cha Eastern and Southern Africa Management Institute alikopata shahada ya kwanza ya mawasiliano ya umma.

Aidha marehemu Mama Rwakatare pia alijiunga na chuo kikuu cha kikristo cha Moody, na safari yake ya kielimu haikuishia hapo, aliendelea hadi kufikia hatua ya udaktari wa falsafa (Philosophy Doctorate- PhD).

Marehemu Mama Rwakatare pia atakumbukwa kwa maneno yake kutoka katika vitabu vitakatifu, ikiwemo upepo wa kisulisuli ambao kwa imani yake alikuwa akiwaombea mabinti ambao hawajaolewa kwamba waume zao watakuja kwa kupeperushwa na upepo huo.

Marehemu Mama Rwakatare pia alikuwa akisifika kwa makongamano na mafundisho ya ndoa, ujasiriamali, malezi pamoja na mafundisho ya Biblia.

Marehemu Mama Rwakatare ni miongoni mwa watumishi wa Mungu waliofanikiwa kujenga majumba ya kifahari jijini Dar es Salaam, yaliyopo Mikocheni B, na nyingine ikiwa ufukweni mwa Bahari ya Hindi huko Mbezi.

Mbali na hayo marehemu Mama Rwakatare, pia alikuwa ni mmiliki wa kituo cha Redio cha Praise Power, shule na vyuo vya St. Mary’s kwenye mikoa mbalimbali chini, vitu ambavyo bado vinaendelea hadi sasa.

Ikumbukwe kuwa marehemu Mama Rwakatare aliwahi kuwa Mbunge wa Viti Maalum wa Mvomero, kuanzia mwaka 2008 hadi 2015, na baadaye aliteuliwa na Rais Dkt. Jakaya Kikwete kuwa mbunge.

Askofu Dkt. Getrude Rwakatare,  alizikwa  Alhamisi ya Aprili 23, 2020, katika viunga vya kanisa lake lililopo Mikocheni B, jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita