Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli alipokuwa ziarani Tabora
Kufuatia agizo hilo tayari SUMATRA kwa kushirikiana na jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani wameanza kuelekeza magari yote ya abiria yanayopita Tabora eneo la stendi hiyo kuhakikisha yanapita jambo ambalo limeanza kufanyiwa kazi kwa vitendo.
Akizungumza wakati wa kukagua utekelezaji wa agizo hilo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri amesema SUMATRA washirikiane na jeshi la polisi kuhakikisha kila gari la abiria linapita na dereva atakayekaidi agizo hilo anyang'anywe leseni.
Ni lazima mabasi yapite hapa stendi na yeyote atakayekaidi SUMATRA chukueni hatua na jeshi la polisi toenio ushirikiano kuhakikisha suala hili linafanikiwa'' Amesema Mwanri.
Aidha kwa upande wao wananchi wamesema watanufaika sana kufuatia stendi hiyo kuanza kufanya kazi kwa kuwa watafanya biashara mbalimbali kuzunguka stendi hiyo.





