Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

“Nilimpoteza mama nikiwa na miaka sita”- Mwijage

Alhamisi , 24th Mei , 2018

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage amewataka wanafamilia, wafanyakazi na watanzania kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu ambapo Taifa limepoteza maofisa watatu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).

Waziri Mwijage amesema hayo leo Mei 24, 2018 katika ibada ya kuaga miili ya waliokuwa wafanyakazi watatu wa kituo cha uwekezaji waliofariki katika ajali ya gari eneo la Msoga na kuongeza kuwa anatambua wakati mgumu wanaopitia familia ya watumishi hao kwa kupoteza wapendwa wao kwasababu hata yeye alimpoteza mama yake akiwa na miaka sita.

“Hakuna zaidi ninaloweza kufanya, familia ni muhimili, uzoefu wangu mbaya hauwezi kuwa nafuu kwenu lakini hawa watoto wadogo wanaweza kufanana na mimi, nilimpoteza mama yangu nikiwa nina miaka sita lakini haya ni mapenzi ya Mungu” amesema Mwijage.

Waziri Mwijage ameongeza kuwa, Taifa limepoteza watu muhimu katika jitihada za kukuza sekta ya uwekezaji nchini na kuwataka wafanyakazi wengine wa kituo hicho kutohuzunika sana bali wawakumbuke wenzao kwa kufanyakazi kwa bidii.

Mei 21, 2018 katika eneo la Msoga mkoani Pwani watumishi watatu wa Kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) walifariki Dunia baada ya gari waliyopanda kugongana na lori walipokuwa wakisafiri kikazi kuelekea Dodoma, waliofariki ni Martin Laurence (39), Zakaria Nalinga (49) na Said Moshi.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa