
Hayo yamesemwa katika mahafali ya chuo cha ujasiriamali na urembo (Maznat Beauty College) ambapo Mkurugenzi Mkuu Maznat amesema kuwa Chuo hicho kwa kushirikiana na wadau wenginee wamefanikisha mafunzo ya ujasiriamali na urembo kwa vijana ambao watakuja kuinuka kiuchumi, kujiendeleza kibiashara na kuinua wengine ili kupunguza wimbi la vijana wasio na ajira.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkuu Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe amesema kuwa serikali itaendelea kuwaunga mkono vijana na kuwawezesha ili waweze kuinuka kiuchumi.