
Kwenye picha ni wataalam wa kampuni ya Meta wakiwa na viongozi wa TRA.
TRA imefanya mazungumzo ya awali na kampuni ya Meta kuhusu namna ya kutoza kodi katika huduma zao nchini. Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam.
TRA wametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wao wa twitter.
#DARESSALAAM Timu ya Wataalam wa Kampuni ya @meta inayomiliki mitandao ya @facebookapp @instagram pamoja na @whatsapp leo 21 Aprili, 2022 imefanya mazungumzo ya awali na TRA kuhusu namna ya kutoza kodi katika huduma zao nchini. Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam. pic.twitter.com/PmqbA69nD2
— TRA Tanzania (@TRATanzania) April 21, 2022