Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Jestas Nyamanga
Kauli hiyo ameitoa hii leo Septemba 21, 2022, wakati akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya mtandao kuhusu fursa mbalimbali kwa Watanzania zilizopo nchini Ubelgiji.
"Tanzania ni ya tatu Ulaya kwa kuuza Parachichi lakini sehemu kubwa ya parachichi letu tunauza kupitia Kenya na tumezungumza na TAHA kuona namna gani tukauza moja kwa moja huku, Parachichi lenye vipelepele lina soko kubwa sana hapa Ulaya," amesema Balozi Jestas
Aidha Balozi ameongeza kuwa, "Parachichi moja inauzwa Euro 4 zaidi ya elfu 10 za Tanzania wakati nyumbani utalinunua kwa shilingi 500 au 1000 sasa ukiuza huku unaweza ukapata faida kubwa mno,".