Jumatatu , 18th Dec , 2023

Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo amesema serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri ya kufanya biashara na uwekezaji pamoja na uhuru wa kufanya biashara kwa watanzania na wawezekaji kutoka nje ili wafanye biashara na kutengeneza fursa kwa watanzania

Amesema lengo la serikali ni kuweka mazingira rafiki ya watu kufanya biashara ambapo amesema ili serikali iendelee kuweka mazingira rafiki amewataka wawezekaji kulipa kodi kwa wakati ili wananchi waendelee kupata maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara na miundombinu mbalimbali 

Profesa Kitila amesema moja ya lengo la serikali la kupunguza Makampuni na kuuganisha baadhi ya kampuni na taasisi ni ili Kupunguza kiwango cha usimamizi ambapo kwasasa taasisi nyingi zilikuwa zinafanya kazi zinazonana