Jumatano , 20th Oct , 2021

Joto la Mpambano lililopewa jina la ''Dar Boxing Derby'' limezidi kupanda kwa miongoni mwa mabondia wanaojiandaa kupanda ulingoni siku ya Oktoba 30, katika uwanja wa Kinesi, Ubungo jijini Dar es salaam.

Mratibu wa mpambano huo Kapteni Suleiman Semunyu.

Akizungumza na EATV, mratibu wa mpambano huo Kapteni Suleiman Semunyu, amesema kuwa mabondia wanajiandaa vizuri kuelekea kwenye ngumi hizo zinazokutanisha wakali wa masumbwi jijni Dar es salaam.

Vile vile, Kapteni Semunyu amesema mabondia wanajifua vikali na vilivyo ili wawezae kutoa burudani kwa mashabiki na wapenzi wamchezo huo.

''Mabondia wanafanya mazoezi ya mwisho, hivyo sisi kama waandaji inatupa faraja kuona mabondia hawa wamelipa tamasha hili uzito wa hali ya juu, mpaka sasa tiketi zimeanza kuuzwa kwaiyo watu wajitokeze kwa wingi wanunue na wajitokeze kinesi” 

Sanjari na hayo, amesema kuwa suala la ulinzi na usalama limeshaandaliwa na kama ilivyo kwenye mapambano mengine, atahakikisha usalama wa kila mtu atakayejitokeza kwenye ukumbi huo unalindwa.

''Mara nyingi, huwa sibahatishi nikiandaa mpambano huwezi kusikia, mtu kaibiwa simu, pochi wala pesa yake, nitaimalisha ulinzi, haya yote ikiwa na lengo la kuhakikisha watu wanakuja Kinesi na Kufurahi mchezo wa ngumi na kupata burudani'' Amesema Semunyu.

Pambano linalosubiriwa na wengi ni lile litakalowakutanisha mabondia Ramadhani Shauri na Iddy Pialari mpambano utakaochezwa Oktoba 30, 2021 kwenye uwanja wa kinesi Jijini Dar es Salaam.