Jumatatu , 15th Dec , 2014

Staa wa Hip Hop hapa Bongo, ROMA amezungumzia utaratibu wake wa kujifananisha na Kiongozi wa Dini, kutumia maudhui ya dini katika kazi zake na pia kunukuu mistari kutoka vitabu vya dini.

mkali wa miondoko ya Hip Hop nchini Roma Mkatoliki

Roma pia amesema kuwa huo ndio utaratibu wake katika kuweka uhalisia katika sanaa yake.

ROMA ameiambia eNewz kuwa, utaratibu huu pia ndio ulioibua jina la ROMA Mkatoliki, na pia ni ubunifu wa kumtofautisha yeye na wasanii wengine, akiwa pia anatumia sanaa yake kuwasaidia mashabiki kiroho.