Alhamisi , 17th Aug , 2017

Mzee mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mzee Msaka amefunga safari kutoka Wazo Hill anakoishi mpaka studio za East Africa Radio kuja kuonana na Big Chawa, kumletea malalamiko yake kuhusu Alikiba.

Mzee huyo amesema anamtaka Alikiba aachie ngoma kali ambazo zitafunika kwa mwaka huu wote, kwani ukimya wake umemchosha.

Mashabiki wa Alikiba wamekuwa wakilalamikia kwa muda mrefu kitendo cha msanii huyo kukaa kimya muda mrefu bila kutoa kazi yoyote, wakati wasanii wenzke wakiachia ngoma kila siku.

Mtazame hapa chini alivyokuwa akimlilia Alikiba