Yaliyojiri Dance 100% mwaka 2013
Msimu wa pili wa mashindano makubwa ya kucheza Africa Mashariki Dance 100% mwaka 2013, yalilitikisa jiji la Dar es Salaam na Tanzania nzima kwa ujumla baada ya makundi yenye ujuzi mkubwa kujitokeza.
Baada ya mchujo kufanyika, makundi matano yaliyopita na kufanikiwa kwenda kwenye fainali ni kundi la The chocolate, DDI Crew, Wakali Sisi, The Winners na The WT.
Makundi yote yalipewa muda wa kujianda vizuri ili kuonesha uwezo wao mkubwa, maana makundi yaliyoingia fainali yalikuwa yana uwezo mkubwa katika uchezaji, hali iliyofanya hadi majaji kuwa makini sana katika kuamua.