Rukwa Yaongoza kwa Wahamiaji Haramu
Zaidi ya wahamiaji haramu 117 waliingia nchini Tanzania kinyume cha sheria mwaka uliopita kupitia mkoani ya Rukwa, na kuufanya mkoa huo kuongoza kwa tatizo kubwa la wimbi la wahamiaji haramu nchini ambao wanatokea katika nchi za jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Burundi, Zambia na zile za Rwanda na Somalia.