Watu 26 wanashikiliwa, kutekwa kwa Mo Dewji
Watu 26 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam akiwemo, Afisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara kwaajili ya uchunguzi zaidi kutokana na tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara Mohammed Dewji ‘Mo’ ambaye pia ni mwekezaji wa klabu hiyo.