Waziri Mkuu aagiza DED kuchunguzwa
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga awasilishe kwake taarifa za utendaji kazi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Waryoba Gunza, baada ya kushindwa kutoa maelezo kuhusu utekelezaji wa mradi wa maji kata ya Rutamba.