Rais Ramaphosa azomewa Zimbabwe, aomba msamaha
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, amewaomba waafrika msamaha pamoja na kuonesha kujuta kwake, kufuatia mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni yaliyotokea siku za hivi karibuni nchini humo na amewakaribisha raia wa mataifa mengine kwenda huko akisema hali hiyo haitotokea tena.

