Rais kupeleka walimu nchi za falme za kiarabu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amekutana na Mtawala wa Ras-Al-Khaimah katika umoja wa nchi za falme za kiarabu, Mtukufu Sheikh Saud Bin Saqr Al Qasimi na kufanya nae mazungumzo yaliyolenga kuendeleza uhusiano katika sekta ya elimu.

