Mikoa mitatu yapewa tahadhari
Mamlaka ya hali ya hewa nchini (TMA), imetoa tahadhari ya mvua kubwa kwa siku mbili mfululizo, kuanzia Oktoba 17 na 18, 2019, katika mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani na Visiwa vya Unguja na Pemba, hali itakayopelekea kusimama kwa muda kwa shughuli za kiuchumi katika maeneo hayo.

