Wasiojulikana wamchukua Tito Magoti
Kufuatia taarifa zilizotolewa leo Disemba 20, 2019, na Mwanaharakati Bob Chacha Wangwe, zimeeleza kuwa Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Tito Magoti, amekamatwa kwa nguvu na watu watano ambao hawakuweza kutambulika mara moja maeneo ya Mwenge, jijini Dar es Salaam.