Kauli ya CHADEMA baada ya Mbowe kuitwa mlevi
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tumaini Makene amesema kuwa chama hicho hakiwezi kujibishana na wale wote waliotoa kauli za kwamba, Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe alilewa na kudondoka na si kushambuliwa kama chama kilivyosema.

