Dkt Gwajima wapa neno wazee
Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalum Dkt Dorothy Gwajima, amewaomba wazee kubadilisha hadithi za kale walizo wasimulia wajukuu zao kuhusiana na Imani za kishirikina na badala yake wakawahadithie hadithi zitakazowajenga na kuwa raia wema kwa taifa.