Real Madrid yapania kuibomoa Arsenal 2025

Jina Beki kisiki wa klabu ya Arsenal ya Uingereza limeibuka kwenye listi ya Florentino Perez Real ambao anataka kuwasajili pindi dirisha kubwa litakapofunguliwa majira ya kiangazi, William Saliba anatajwa kama mmoja wa Walinzi bora wa kati kwa sasa Duniani Raisi wa Los Blancos anaona Saliba atakuwa tiba ya safu ya Ulinzi ya mabingwa hao watetezi wa La Liga kwa muda mrefu
Real Madrid ya Hispania imepania kumsajili mlinzi wa kati wa klabu ya Arsenal raia wa Ufaransa William Saliba ili kuimarisha safu yao ya ulinzi inayomtegemea zaidi Antoni Rudiger, Saliba anatizamwa kama mrithi sahihi wa Kepteni wao wa zamani Sergio Ramos.