Saturday , 21st Mar , 2026

Msanii Asake amenyoosha maelezo kuwa Msanii Olamide ataendelea kuwa na nafasi kubwa katika maisha yake siku zote hata kama atakuwa Rais wa Marekani bado ataendelea kumuheshimu Legend huyo kutoka Nchini Nigeria Olamide.

Asake ameeleza hayo alipokuwa akifanya mahojiano kwenye moja ya podcast huko nchini Nigeria.

Ikimbukwe kuwa Asake alitolewa kimuziki na Label ya msanii Olamide YBNL mwaka 2022 na kufanya naye kazi kwa ukubwa sana na baadae mwaka 2025 Asake alitangaza kuachana na Label hiyo.

Hivyo kauli hii ya Asake imeendelea kuonesha heshima kubwa kwa Olamide licha ya wawili kuacha kufanya kazi pamoja.