
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro amethibitisha kwa njia ya simu na kuwaeleza waandishi wa habari waliopo eneo la tukio kuwa mwili mwingine mmoja wa kijana Magumba Ngondi (28) umeopolewa huku akiwa amefariki.
"Mwili wa marehemu ulioopolewa leo umehifadhiwa katika chumba cha maiti katika hospitaliya wilaya iliyopo Iselamagazi, lakini pia zoezi la uokoaji linaendelea," amesema Mtatiro
Amesema vikosi vya uokoaji tangu juzi viliungana vikiwemo kikosi cha zimamoto, Msalaba mwekundu na Uokoaji kutoka Mgodi wa Barrick Bulyanhulu
Katika tukio hilo jumla ya watu 25 walibainika kufukiwa na kifusi katika mgodi huo mpaka sasa watu watatu wameokolewa na hali zao ni nzuri, huku wawili ambao ni Emanuel Kija na Magumba Ngondi wamefariki #EastAfricaTV