Wednesday , 11th Jun , 2025

Serikali ya Marekani imeanza rasmi utekelezaji wa amri ya kutotoka nje kwa wananchi wa jiji Los Angeles ikiwa ni njia ya kuzuia uharibifu unaoendelea

Meya wa Los Angeles Karen Bass ametangaza amri hiyo ya kutotoka nje katika jiji Los Angeles kukomesha uharibifu.
Bass amesema amri ya kutotoka nje itatekelezwa kuanzia saa mbili usiku hadi saa kumi na mbili asubuhi.

Akielezea hitaji la amri ya kutotoka nje, na kuongeza kwamba kumekuwa na "uharibifu mkubwa" katika jiji lote.
Mkuu wa polisi wa LA Jim McDonnell, alisema amri ya kutotoka nje ni hatua muhimu ili kuokoa maisha na kulinda mali baada ya mfululizo wa machafuko yanayoongezeka katika jiji hilo.

Alisisitiza kuwa watu watakaovunja amri ya kutotoka nje bila upendeleo watakamatwa.

Bass alisisitiza maneno yake ya awali - kwamba anataka Trump asitishe hatua ya kutumiwa kwa wanajeshi katika jiji hilo.

Wakati huo huo, Jaji wa Marekani alizuia ombi la dharura kutoka kwa Gavana wa California la kutaka kuzuia kutumiwa kwa wanajeshi kwenye vurugu zilizoshuhudiwa katika mji wa Los Angeles.

Gavana Gavin Newsom ameitaja hatua hiyo kuwa kinyume na sheria.

Rais Donald Trump ametetea uamuzi wake wa kutuma majeshi kukabiliana na waandamanaji wanaopinga sera kali dhidi ya wahamiaji na kuapa kuwa kamwe hataruhusu mji wowote wa Marekani kuvamiwa na kutawaliwa na wageni.