
Magari yaliyokwama barabarani
Baadhi ya abiria wamesema kuwa magari kadhaa yameshindwa kupita katika eneo hilo baada ya barabara hiyo kujaa tope na maji, hali iliyosababisha msongamano mkubwa wa vyombo vya usafiri.
"Mvua iliyonyesha kuanzia saa 7:00 usiku imesababisha barabara kuharibika na magari yaliyopo hapa ni ya kuanzia muda huo, imetuletea shida watu wanakwama kusafiri wengine tunaenda kazini," amesema Jonson Mulokozi
Mpaka sasa juhudi za kuhakikisha magari yanapita zinaendelea huku tayari magari yameanza kupita chini ya uangalizi wa mkandarasi aliyepewa ujenzi wa daraja eneo hilo huku jeshi la polisi wakizidisha ulinzi kutokana na msongamano uliopo