Monday , 24th Mar , 2025

Chelsea italazimika kuilipa Manchester United ada ya pauni £5m ambazo ni zaidi ya bilioni 14 za Tanzania iwapo itaamua kutomsajili Jadon Sancho kwa mkataba wa kudumu msimu huu wa joto.

Jadon Sancho na Cole Palmer

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alijiunga na Chelsea kwa mkopo mwezi Agosti katika mkataba ambao ulijumuisha kipengele cha kumnunua kati ya £20m na ​​£25m, endapo klabu hiyo ya London itamaliza angalau nafasi ya 14 kwenye Premier League msimu huu.

Chelsea wanashika nafasi ya nne, huku kukiwa na mechi tisa mkononi. Hata hivyo, kwa mujibu wa Athletic, kuna vyanzo vinavyofahamu kuhusu mkataba huo kwamba kuna kipengele kinachoiruhusu Chelsea kumrudisha Sancho Old Trafford mradi tu wailipe United £5m kama fidia.

Chelsea hapo awali walisisitiza kuwa hawafikirii kumuachia Nyota huyo lakini shaka imeanza baada ya Sancho kutokuwa na mwenendo nzuri Stamford Bridge akiwa amechangia asisti moja pekee katika mechi 18 tangu kufunga goli la mwisho kati ya mabao yake mawili dhidi ya Tottenham Desemba 08/2024.