Sunday , 23rd Mar , 2025

Nahodha wa timu ya Taifa ya Ureno na Klabu ya Al Nassr ya nchini Saudia Cristiano Ronaldo ameweka wazi malengo yake ndani ya kikosi cha Ureno ni kuona Timu inashinda na siyo yeye kufunga tu.

Cristiano Ronaldo - Nahodha wa kikosi cha Ureno

“Nataka Ureno ishinde, nataka kutetea Bendera ya Nchi yangu mpaka nitakapo kufa. Nitafurahi sana kama leo tutashinda, hata akifunga mchezaji mwingine tofauti na mimi nitafurahi kwasababu lengo letu ni ushindi”

“Kuhusu Hojlund kufunga na kushangilia kama mimi kwangi siyo tatizo, siyo yeye tu watu wengi wamekuwa wakishangilia kwa staili yangu. Leo nitamuonyesha namna ya kuishangilia nitakapofunga” – Cristiano Ronaldo

Portugal Itashuka dimbani leo kukabiliana na Denmark majira ya saa 4:45 usiku kujaribu kulipa kisasi baada ya kupoteza mchezo wa kwanza ugenini kwa kufunga 1-0 goli lililofungwa na mshambuliaji wa Manchester United Rasmus Hojlund