Tuesday , 18th Feb , 2025

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, imefanikiwa kuteketeza ekari 336 za mashamba ya bangi pamoja na mirungi kilogramu 148, yaliyokuwa ndani ya hifadhi ya Ikome wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma yakiwa yamechanganywa na mazao mengine.

Shamaba la bangi likiteketezwa

Akiongea mara baada ya operesheni hiyo, Kamishna Jenerali wa Mamlaka hiyo Aretas Lyimo amesema operesheni hiyo ni hatua kubwa ya vita dhidi ya dawa za kulevya.

"Hii ni operesheni kubwa ya kwanza kufanyika mkoani Dodoma, ikionyesha wazi kuwa kilimo cha bangi kimeanza kuenea katika baadhi ya maeneo ya mkoa huu tutaendelea kuchukua hatua kali kuhakikisha kuwa uzalishaji, biashara na matumizi ya dawa za kulevya vinadhibitiwa kwa nguvu zote," amesema Aretas Lyimo Kamishna DCEA.

Aidha Lyimo amesema katika kipindi cha Januari hadi Februari 2025 wamefanikiwa kukamata kilogramu 790.5 za aina mbalimbali ya dawa za kulevya pamoja na watuhumiwa 114 kwa tuhuma za biashara hiyo haramu.