Monday , 17th Feb , 2025

Pep Guardiola anaamini kuwa Manchester City wana nafasi ya asilimia 1% tu ya kushinda katika mechi ya mkondo wa pili na kuwaondoa Real Madrid kwenye Ligi ya Mabingwa hapo kesho Jumatano.

Pep Guardiola - Kocha wa Manchester City na Earling Haaland

City wanakwenda Santiago Bernabeu wakitoka kushinda 4-0 dhidi ya Newcastle United. Ikumbukwe mchezo wa mkondo wa kwanza Man City walipoteza 3-2 katika Uwanja wa nyumbani ya wiki jana.

"Upeo wa kushinda Bernabeu katika nafasi hiyo, kila mtu anajua kwamba ukiniuliza kabla ya mchezo, asilimia ya kushinda na kupita, sijui ila tunafika 1%," Guardiola amesema.

Katika michezo 10 ya mwisho timu hizi kukutana Manchester City wameshinda michezo 5 huku Real Madrid wakishinda michezo 3 na kutoa  sare katika michezo 2.