Wednesday , 9th Oct , 2024

Safari ya miaka sita kitandani imekuwa ni hadithi ndefu, anasema kila siku moja yenye saa 24 kwake ni sawa na saa 48 kwa maumivu makali anayopitia.

Mwanahawa Shomari

Simulizi ya mama huyu aitwaye Mwanahawa Shomari, mkazi wa Tegeta Wazo jijini Dar es Salaam anayesumbuliwa na magonjwa ya Figo, Ini na Moyo ilianza kuwa ngumu tangu mtoto wake wa kiume alipoamua kumtelekeza na sasa anakaa kwa mwanae wa kike ambaye pia hali yake ya maisha si nzuri.

Mama huyu anasimulia kuwa  amekosa pesa ya kwenda hospitali kufanyiwa vipimo zaidi na kuanza matibabu, hivyo kuomba watanzania watakaoguswa kumchangia ili apate tumaini la kunyanyuka tena kitandani hapo.

Mawasiliano ya kumpata ama kumtumia chochote ni kupitia namba ya bintiye, 0714842036 jina Amina Mwinshehe.