Monday , 23rd Sep , 2024

Mlinda mlango wa FC Barcelona Marc Andre ter Stegen atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi 8 baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti Leo jioni Septemba 23, 2024. Ter Stegen aliumia jana kwenye mchezo wa Ligi kuu Hisapania La Liga dhidi ya Villarreal mchezo ambao Barcelona iliibuka na ushindi

Baada ya upasuaji huo Ter Stegen raia wa Ujerumani anatarajia kurejea tena uwanjani Aprili au Mei 2025. Alipata jeraha hilo la goti baada ya kudondoka vibaya wakati akiokoa mpira wa krosi uliopigwa na Villarreal dakika ya 45 ya mchezo huo.