
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete
Amesema kutokana na uzito huo serikali kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao imeamua kusanifu, kujenga na kusanikisha Mfumo wa Kitaifa wa Kielektroniki wa Ununuzi Tanzania {National e-Procurement System of Tanzania (NeST)} ili kuweza kukabiliana na changamoto hiyo.
Ametoa kauli hiyo leo Jijini Arusha wakati akifunga kongamano la 14 la mwaka la wataalam wa ununuzi na ugavi zaidi ya 900 lenye kauli mbiu "Mabadiliko ya kidijitali kwa ajili ya kuboresha usimamizi na ugavi kelekea maendeleo endelevu"
Amesema mfumo huo utasaidia kuondoa mianya ya rushwa na upendeleo na hivyo thamani ya pesa za Serikali katika bidhaa na huduma italindwa kwani kutakuwa hakuna ulazima wa watu kukutana ana kwa ana
"Ni furaha yangu mimi kama Naibu Waziri ninayeshughulikia Utawala Bora ambapo ninasimamia uzuiaji na mapambano dhidi ya rushwa, naamini mfumo huu utaondoa hisia hasi zilizojengeka katika jamii kwenye suala la manunuzi ya umma na hivyo kuongeza uwazi," amesema Mhe.Kikwete
Mhe.Kikwete amesema mfumo huo utaongeza ufanisi, uwazi na ushindani katika ununuzi wa umma.
Katika hatua nyingine, Mhe.Kikwete amesema serikali haitamvumilia mtu yeyote atakayesababisha upotevu wa rasilimali za nchi huku akiwataka wasithubutu kucheza na mfumo huo mpya wa manunuzi kwa umma.