
Katika moto huo uliotokea asubuhi la leo Desemba 1/2023 watu watano wamenusurika kifo akiwemo mtoto aliyekuwa anajiandaa kwenda shule
Akiongea na EATV mmiliki wa nyumba hiyo Gabriel Makupa anasema moto ulianza kwenye chumba cha dada wa kazi na baadae ukaenea nyumba nzima na walijitahidi kuumiza lakini hawakufanikiwa mpaka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lilivyofika.
Akielezea mali zilizoungua anasema hakuna kitu chochote walichofanikiwa kuokoa isipokuwa watu wote waliopo ndani walitoka salama.
Mali zilizoteketea ni pamoja na Camera za picha zaidi ya nane, vifaa vyote vya ndani na moja ya gari imeungua kidogo