
Waziri wa Madini wa Malawi, Monica Chang'anamuno (kushoto) akimkabidhi tuzo ya mshindi wa jumla katika kipengele cha uhifadhi mazingira, afya na usalama mahala pa kazi, Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong. Kulia ni Waziri wa Madini, Anthony Mavunde. Hafla hiyo iliyofanyika wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.
kutokana na jitihada zake katika uwajibikaji kwa jamii pamoja na kuzingatia afya na usalama mahala pa kazi.
Hatua hiyo inatokana na Kampuni hiyo kushinda tuzo mbili ambazo ni mshindi wa jumla katika kipengele cha Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) pamoja na uhifadhi wa mazingira, afya na usalama kazini. Tuzo hizo zilizotolewa na Wizara ya Madini zimeendelea kudhihirisha hadhi ya GGML kuwa mfano wa kuigwa katika masuala hayo ya afya na usalama kazini pamoja na kukuza uchumi wa Taifa.
Waziri wa Madini wa Serikali ya Malawi, Monica Chang'anamuno akiongozana na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde alikabidhi tuzo hizo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong pamoja na Makamu Rais wa AngloGold Ashanti- GGML anayeshughulikia miradi endelevu Ghana na Tanzania, Simon Shayo.
Hafla hiyo iliyopewa jina la Usiku wa Madini, ilifanyika tarehe 25 Oktoba 2023 jijini Dar es salaam.
.jpg?itok=TGpNgU93)