
Baadhi ya blanketi na godoro zitakazogawiwa kwa wananchi waliopata maafa
Mvua iliyoambatana na upepo mkali imenyesha alfajiri ya leo Oktoba 18, 2023, huku zaidi ya nyumba 100 zikiezuliwa paa zake na upepo na kupelekea kifo cha mtu mmoja, ambapo wakazi wa Kata ya Rwamishenyi, Hamugembe na Kashai ndiyo wameathirika zaidi na mvua hizo.
Aidha kufuatia mvua iliyonyesha Oktoba 16 mwaka huu, zaidi ya nyumba 150 na vyumba vya madarasa 20 viliezuliwa na upepo, huku mashamba ya baadhi ya wananchi wa Kata ya Karambi wilaya ya Muleba mkoani Kagera yakiathiriwa.