Mkurugenzi wa Michezo, Ally Mayai amesema Watanzania wamezoea kutangaziwa kikosi na sio njia ya sasa ambayo wameshtukia timu tayari ipo kambini kujiandaa na mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Sudan ambao usiku wa jana umemalizika kwa sare 1-1.
''Ninaaamini TFF italifanyia kazi suala hili ili warudshe ule utaratibu uliokuwepo mwanzo utakaowasaidia watanzania kuifahamu timu yao ili wapate muda wa kumchambua mchezaji mmojammoja,'' amesema Tembele
Katika hatua nyingine Tembele amekipongeza kikosi cha timu hiyo kwa kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Sudan kwenye mchezo wa kirafiki wa Kimataifa ambao umechezwa Jumapili ya jana Oktoba 15, 2023 nchini Saudi Arabia.
''Wachezaji walionyesha uwezo ambao kocha wao Mkuu tayari amepata na kuona kile alichokuwa anakihitaji.''amesema Tembele.
Ikumbukwe Stars ipo tayari na harakati za kuwania tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia katika fainali zitakazofanyika 2026 katika nchi za Canada, Marekani na Mexico ambapo mechi zake za kuwania kufuzu zitaanza mwezi ujao.