Friday , 13th Oct , 2023

Mahakama ya wilaya Manyoni mkoani Singida imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela pamoja na fidia ya shilingi milioni 2, Mlanda Yohana mwenye umri wa miaka 33 mkazi wa Kijiji cha Chibumagwa wilayani humo, kwa kukutwa na kosa la kufanya tendo la ndoa na mtoto wake wa kumzaa.

Baba aliyehukumiwa miaka 30 jela

Akisoma hukumu hiyo namba 114 ya mwaka 2023, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya Manyoni Alisile Mwankejela, amesema kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo usiku wa tarehe 03/07/2023 wakiwa nyumbani kwake huko kijiji cha Chibumagwa Kata ya Msakile.

Amesema kuwa  siku ya tukio mshtakiwa alimwambia binti yake aingie ndani akalale na yeye kufunga mlango, kisha akaingia ndani kwa binti yake huyo mwenye umri wa miaka 14.

Baada ya kuingia chumbani binti akawasha tochi na akamuona baba yake kisha akaanza kufanya tendo hilo, ilipofika asubuhi ya tarehe 03/07/2023 binti akaanza kuhisi maumivu ndipo akaamua kwenda kwa jirani ambaye ni shahidi namba 3 kuelezea tukio hilo ndipo wakaenda ofisi ya mtadaji kutoa taarifa.

Mwankejela akiendelea kusoma hukumu hiyo amesema baada ya kufikishwa katika mahakama hiyo mshtakiwa alipotakiwa kutoa utetezi na kumuuuliza swali mhanga wa tukio hilo ambaye ni mtoto wake mshtakiwa alishindwa kuuliza swali lolote hali ambayo ilionesha wanafahamiana.

Huku mshtakiwa akisema kuwa mtoto wake alikuwa anaota kufanyiwa tendo hilo na amekuwa na uhasama nae kwa kile alichodai kutaka kwenda kuishi kwa ndugu upande wa mama yake jambo ambalo mahakama ililitupilia mbali kwa kukosa mashiko.