Friday , 13th Oct , 2023

Mwili wa mwanafunzi Nyangige Chacha  aliyefariki kwa kutumbukia katika shimo lililochimbwa kwa ajili ya Ujenzi wa choo katika kituo cha afya Gibaso umezikwa leo Oktoba 13 baada ya walimu kukubali kugharamia gharama zote za mazishi

Awali wazazi pamoja na wananchi waligoma kuzika mwili wa mwanafunzi huyo kufuatia kile kilichodaiwa kuwa mwanafunzi huyo  alitumwa maji na mwalimu wa shule huyo kwa ajili ya matumizi yake huku wakiiomba serikali kugharamikia mazishi baada ya mwalimu kutoonyesha ushirikiano kwao

Aidha Kaka wa Marehemu Mwita Gibuka amethibitisha kuwa tayari familia hiyo imekaa pamoja na Uongozi wa shule hiyo na kusuluhisha tatizo na tayari wako tayari kuzika baada ya kusaidiwa kugharamikia mazishi ya Marehemu binti yao

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kitongoji cha Makonge Kijiji cha Gibaso  kilichopo kata ya Kwihancha Mwita Gasaya ambapo ndipo nyumbani kwao marehemu anaeleza  kuwa mpaka Sasa  hali ni tulivu na jamii imeshiriki kikamilifu katika mazishi hayo