Thursday , 12th Oct , 2023

Wananchi wa Wilaya  ya Kilindi Mkoani Tanga  wamemlilia  mlezi wa CCM Mkoa wa Tanga ambaye ni Makamu wa pili wa Rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Hemed Suleiman Abdala  dhidi ya mgogoro wao wa mpaka kati ya wilaya ya Kilindi na Kiteto mkoani Manyara uliodumu kwa muda mrefu sasa. 

Wananchi wa Wilaya  ya Kilindi Mkoani Tanga  wamemlilia  mlezi wa CCM Mkoa wa Tanga ambaye ni Makamu wa pili wa Rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Hemed Suleiman Abdala  dhidi ya mgogoro wao wa mpaka kati ya wilaya ya Kilindi na Kiteto mkoani Manyara uliodumu kwa muda mrefu sasa. 

Wakizungumza mbele ya Mlezi wa chama hicho Hemed Suleiman Abdulla  viongozi wa wilaya ya kilindi wanaomba kuharakishwa kwa mchakato wa mpaka huo  ili kuepukana na  migogogro  kati ya wakulima na wafugaji .

"Mgogoro wa mpaka kati ya Kilindi na Kiteto mlezi wetu mgogoro huu tunasema ni mdogo kwasababu waziri Mkuu alishafika akatoa maelekezo wapimaji wamepita kilichobakia ni kusoma GN peke ake na kuweka mipaka ili kila mmoja ajue mpaka wake, "alisema 

Mbunge wa jimbo la Kilindi Omari Kigua  alisema jambo hilo limekuwa likileta usumbufu mkubwa hasa kwa viongozi wa serikali kwa kuwa wamekuwa hawasimamii miradi ya maendeleo kwajili ya migogoro ya kila siku kati ya wafugaji na wakulima. 

"Suluhu ya kudumu ya jambo hili ni kuweka alama kubainisha eneo la mpaka kati ya kiteto na Kilindi kwa kuwa wote ni watanzania watu wa Kiteto wote ni Wanguu, wamasai na tulikuwa tukiishi kwa amani kwa muda mrefu hivyo tunaomba jambo hili lifanyiwe kazi kwa haraka, "alisema.

Katika majibu yake Mlezi wa Chama hicho Makamu wa pili wa Rais Zanzibar ameahidi kuharakisha mchakato wa kupatikana kwa mpaka huo kumaliza mgogogro huo uliodumu kwa muda mrefu.

Makamu wa pili wa Rais amesema kuwa suala hilo la mpaka kati ya Kilindi na Kiteto inakwenda kumalizika kwa haraka iwezekanavyo kwa kuwa juhudi kubwa zinaendelea kuchukuliwa na serikali ili kumaliza tatizo hilo. 

"Niwaombe sana wanakilindi tuendelee kuwa watulivu na kudumisha amani tukiamini serikali yetu ya chama cha mapinduzi inapenda sana wananchi wake waishi vizuri na jambo hili la migogoro watanzania wote hatulipendelei liendelee kubaki bila ya kupatiwa ufumbuzi kwakuwa athari yake tumeshaiyona siku hadi siku, "alisisitiza Makamu wa pili wa Rais. 

Mgogogro huo umekuwa ukisababisha usumbufu  kwa viongozi wa serikasli pale ambapo wanashindwa kusimamia miradi ya maendeleo  wakijikita kwenye migogogro ya wakulima na wafugaji ambayo imekuwa ikihatarisha maisha kati ya jamii hizo