![](http://eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2023/10/10/Snapinsta.app_354699707_793164802349753_5036848353159234438_n_1080.jpg?itok=SBnbKfUx×tamp=1696952478)
Akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari Katibu Mkuu wa TPBRC, George Lukindo amesema, mbali na adhabu hiyo Mwakinyo ameamriwa kulipa faini ya Shillingi Milioni 1 na adhabu hiyo inaanza leo Oktoba 10 mwaka 2023 na kumalizika Oktoba 10 mwaka 2024.
“Walikaa na kuzungumza na pande zote mbili na kubaini kuwa vielelezo na maelezo ya Mwakinyo hayakuwa na sababu zenye mashiko hivyo kulazimika kumuadhibu, Mwakinyo amepewa adhabu hiyo baada ya kuonekana kukiuka taratibu za mkataba wake dhidi ya Promota Godson Karigo,amesema Silas.
Mwakinyo amepewa nafasi ya kukata rufaa ndani ya kipindi cha siku 7 kuanzia siku ya kutangazwa hukumu hiyo.