Akitoa tambo hizo Mkurugenzi Habari na Mawasiliano, Azam FC Thabit Zakaria maarufu 'Zaka za Kazi' amefurahi kuona katika mechi mbili walizocheza katika uwanja wao nyumbani wa Azam Complex Chamazi wamepata matokeo mazuri hivyo amepata imani kubwa.
''“Tunawatumia Salamu Klabu zote ambazo zitakuja kucheza Chamazi katika uwanja wetu lazim waache alama tatu kwani tumedhamiria kutokana na muunganyiko wa kikosi chetu kwa sasa”amesema Thabit Zakaria
Kwa upande mwingine:'Zaka za Kazi' amewataka mashabiki na wapenzi wa Azam FC kuwa wa moja katika kipindi hiki licha ya wao kutolewa katika mikwaju ya Penati 4- 3 katika michuano ya Kombe la shirikisho barani Afrika dhidi Bahir Dar ya Ethiopia.