
Beijing ilijibu kwa kusema majirani zake wanapaswa kujiepusha na "kutafsiri zaidi" suala hilo.
Wakati huo huo, ripoti za vyombo vya habari zinasema Rais Xi Jinping wa China huenda asifanye mazungumzo ya viongozi wa G20 wiki ijayo mjini Delhi.
Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinaashiria kuwa waziri mkuu Li Quang atahudhuria mkutano huo. Bwana Xi awali alithibitisha kuwa atasafiri kwenda Delhi kwa mkutano huo kuanzia Septemba 9-10 - lakini wizara ya mambo ya nje ya China haitathibitisha kuhudhuria kwake alipotakiwa kufanya hivyo katika mkutano wa kawaida na waandishi wa habari siku ya Alhamisi.
India sio nchi pekee inayopinga ramani hiyo ,siku ya Alhamisi, Ufilipino na Malaysia zilitoa maandamano dhidi ya madai ya China ya umiliki wa sehemu kubwa ya bahari ya kusini mwa China katika ramani. Taiwan ambayo China inasema ni jimbo lililojitenga ambalo hatimaye litakuwa chini ya udhibiti wa Beijing pia ilipinga kuingizwa kwake katika ramani.