
Kutokana na tukio hilo la kikatili kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Kilosa ikiongozwa na Mkuu wa wilaya hiyo Shaka Hamdu Shaka, kumtembelea mtoto huyo aliyelazwa katika hospitali ya Mtakatifu Joseph Dumila ili kuona anavyoendelea.
"Namuagiza Mkurugenzi kuhakikisha mtendaji wa Kata pamoja na Afisa Ustawi wa Jamii wa Kata husika wanakamatwa kwa kutoshughulikia hali ya mtoto wakati walipata taarifa na naagiza pia kukamatwa kwa shangazi na mjomba wa mtoto popote walipo," amesema DC Shaka.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi hospitali ya Mtakatifu Joseph Dkt Selemani Sakoro, na msamaria aliyejitolea kumsaidia mtoto huyo Bi Caroline Makemo nao wakaeleza hali aliyokuwa nayo mtoto huyo.
Na hapa Mkuu wa mkuu wa mkoa wa Morogoro Adam Malima, amelaani vikali juu ya tukio hilo la ukatili kwa mtoto huo.