Gari iliyopata ajali
Wakizungumza na #EastAfricaTV baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wanasema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi ambapo gari lilipofika katika kona lilimshinda dereva na kuanguka mtaroni.
"Sisi tulikuwa tumekaa pembeni ya mwa barabara ambapo tuliliona gari hilo likija kwa mwendokasi lakini alipotaka kukata kona ikamshinda na kuanguka," amesema shuhuda
Kwa uapande wao baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo wameelezea namna ambavyo ajali hiyo imetokea.
Akithibitisha kupokea majeruhi wa ajali hiyo Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Bunda Pendo Faustine, amesema wamepokea majeruhi 46 na maiti moja huku mkuu wa wilaya ya Bunda Vincent Naano akiwaonya madereva juu ya mwendokasi.