Tuesday , 4th Jul , 2023

Jeshi la Polisi wilayani Kiteto mkoani Manyara linawashikilia watu 9 wa jamii ya kifugaji Maasai wa Kijiji cha Lengatei kwa tuhuma za kumjeruhi Afisa Mtendaji wa Kata hiyo Julias Kerato na mgambo Ramadhani Ndegule kwa fimbo na marungu wakiwa katika majukumu ya kiserikali.

Wamaasai waliofikishwa mahakamani

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Manyara ACP George Katabazi, amethibitisha tukio hilo na kueleza kuwa uchunguzi unaendelea dhidi ya tukio hilo.

East Africa TV imezungumza na Diwani wa Kata ya Lengateti Hamis Sempela, ambaye naye alinusurika kichapo hicho  huku mmoja wa wananchi hao akitaja sababu watu kujichukulia sheria mkononi