Monday , 3rd Oct , 2022

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne Muliro, amesema kwamba vikundi vya panya road vimekuwepo tangu zamani kwa kuibuka kwa nyakati tofauti tofauti na kuwa na majina tofauti lakini vimekuwa vikifanya matukio yale yale ya uporaji na kujeruhi.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne Muliro

Kauli hiyo ameitoa hii leo Oktoba 3, 2022, wakati akizungumza kwenye mkutano uliowakutanisha Makamanda wa Polisi wa takribani mikoa minne, kuzungumzia hali ya usalama katika mikoa yao na namna ya kudhibiti vikundi vya uhalifu.

"Haya makundi kwa nyakati tofauti tofauti yalikuwa na majina tofauti, kuna kipindi hawa panya road walikuwa wanaitwa komando yoso, baadaye wakawa wanaitwa kiboko msheli, kuna kipindi makundi na watu wenye hulka hii hii walikuwa wanaitwa kumi ndani, kumi nje," amesema Kamanda Muliro

Tazama video hapa chini kwa undani zaidi