Saturday , 9th Jul , 2022

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu George Simbachawene, ametoa rai kwa wananchi kujiandaa kwa zoezi la sensa ya watu na makazi kwa kuwa na kumbukumbu ya taarifa  za watu waliolala katika makazi yako usiku wa kuamkia Oktoba 23, 2022.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, George Simbachawene

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu George Simbachawene, wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Mbuga jimbo la Kibakwe Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.

"Hata kama watu watatoka ni vizuri akabaki mtu mwenye kumbukumbuku za watu waliolala katika nyumba yake ili kupata takwimu sahihi," amesema waziri Simbachawene

Katika hatua nyingine Waziri Simbachawene, ameeleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwaka mmoja wa Rais wa awamu ya sita Samia Suluhu Hassan, na kutoa kiasi cha shilingi million 100 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo elimu na barabara.